Usalama na ulinzi wako na wa jumbe zako zinatuhusu. Tunataka ujue kuhusu zana na vipengele ambavyo tumeunda kukusaidia kukaa salama wakati wa unapotumia WhatsApp. Tunatoa viungo vingine za rasilimali nyingine ambazo zinaweza kukusaidia kukaa salama mtandaoni kwa kawaida.
Njia moja tunayowasaidia kukaa salama kwenye WhatsApp ni kwa Masharti Yetu ya Huduma. Masharti Yetu ya Huduma yametaja shughuli ambazo ni marufuku kwenye WhatsApp. Kwa mfano, kuwasilisha maudhui (katika hadhi, picha za jalada au jumbe) ambazo sio halali, haramu, vibaya, kupotosha, kutishia, kunyanyasa, kuvuruga, chuki, kuchukiza kirangi au kikabila, au kuhamasisha au kuhimiza tabia ambayo ni kinyume cha sheria, au haifai inakiuka Masharti yetu ya Huduma. Tutampiga marufuku mtumiaji ikiwa tunaamini kwamba mtumiaji anakiuka Masharti ya Huduma yetu.
Kwa habari zaidi kuhusu mifano ya shughuli zinazokiuka Masharti ya Huduma yetu, tafadhali kagua "Matumizi Inayokubalika ya Huduma Yetu" kwenye Masharti ya Huduma.
Kwenye WhatsApp, tumeunda udhibiti fulani wa msingi ambao unaweza kurekebisha kama unavyofaa kukusaidia kujilinda::
Unaweza kuweka mwisho kaonwa, picha ya jalada na/au hadhi kwa hiari zifuatazo:
Kila mtu: Mwisho kaonwa yako, picha ya jalada na/au hadhi zitapatikana kwa watumiaji wote wa WhatsApp.
Waasiliani wangu: Mwisho kaonwa yako, picha ya jalada na/au hadhi zitapatikana kwa waasiliani walio kwenye kitabu chako cha anwani tu.
Hakuna: Mwisho kaonwa yako, picha ya jalada na/au hadhi hazitapatikana kwa mtu yoyote .
Ukizima Taarifa za kusomwa, hautatuma taarifa za kusomwa. Pia hautaweza kuona taarifa za kusomwa za wengine.
Kumbuka: Taarifa za Kusomwa hutumwa kwa soga za kikundi, hata kama umezima hiari hiyo kwenye mipangilio ya faragha yako.
Jifunze kuhusu mipangilio ya faragha kwenye: Android | iPhone
Unaweza kuzuia waasiliani maalum kutoshirikiana nawe kwenye WhatsApp. Kwa habari zaidi kuhusu jinsi ya kuzuia/kuruhusu mwasiliani na kujifunza kinachotokea unapozuia mwasiliani tafadhali kagua makala haya.
Unaweza pia kuamua nini cha kushiriki na waasiliani wako kwenye WhatsApp, na tunawahimiza kufikiria kwa makini kabla ya kuamua kushiriki kitu. Jiulize: ungependa wengine waweze kuona kile ulichotuma?
Tafadhali shauriwa ya kwamba hatuhifadhi jumbe baada ya kupokelewa, kwa ukawaida ya kutoa huduma yetu. Mara ujumbe unapopokelewa kwenye WhatsApp, ili kusaidia kuhakikisha usalama, usiri na ulinzi wa jumbe unazotuma hatuhifadhi ujumbe.
Hata hivyo, unaposhirikisha soga, picha, video, faili au ujumbe wa sauti na mtu mwingine kwenye WhatsApp, watakuwa na nakala za jumbe hizo. Wana uwezo wa kushirikisha tena jumbe hizo na wengine ndani na ndani ya WhatsApp.
WhatsApp pia ina kipengele cha eneo ambacho unaweza kutumia ili ushirikisha mahali pako pa sasa mahali kwa kupitia ujumbe wa WhatsApp. Unapaswa kushiriki mahali pako na watu unaowaamini tu.
Unaweza kutuma ripoti kwa WhatsApp kwa kuwasiliana na sisi kutoka ndani ya programu.
Tafadhali toa maelezo mengi iwezekanavyo.
Muhimu: Ikiwa unajisikia kuwa wewe au mtu mwingine yuko katika hatari ya kihisia au kimwili, tafadhali wasiliana na mamlaka yako ya kutekeleza sheria. Wanaweza kusaidia zaidi katika kesi hizi.
Tunakuhimiza kuripoti maudhui ya shida kwetu. Tafadhali kumbuka kwamba ili kusaidia kuhakikisha usalama, usiri na ulinzi wa jumbe zako, kwa ujumla hatuna maudhui za jumbe ambazo hizo, hii hupunguza uwezo wetu wa kuthibitisha ripoti na kuchukua hatua.
Ikiwa inahitajika, unaweza kuchukua skrini ya maudhui na kuishirikisha, pamoja na maelezo yoyote ya mawasiliano yanayopatikana, na mamlaka husika ya kutekeleza sheria.
Unapopokea ujumbe kutoka kwa nambari isiyojulikana kwa mara ya kwanza, utakuwa na chaguo la kuripoti nambari moja kwa moja ndani ya soga.
Unaweza pia kutoa ripoti ya mwasiliani au kikundi kutoka kwa maelezo ya jalada kwa kutumia hatua zifuatazo:
Mara baada ya kuripotiwa, WhatsApp inapokea jumbe za hivi karibuni zilizotumwa kwako na mtumiaji aliyeripotiwa au kikundi, pamoja na maelezo juu ya ushirikiano wako wa hivi karibuni na mtumiaji aliyeripotiwa.
Tunaweza kupiga marufuku akaunti ikiwa tunaamini shughuli ya akaunti inakiuka Masharti ya Huduma yetu. Ilivyo kwenye Masharti ya Huduma, tuna haki ya kupiga marufuku bila taarifa. Tafadhali tahadhari kuwa ripoti ya mtumiaji ya ukiukaji wa Masharti ya Huduma yetu haitatokana na sisi kupiga marufuku mtumiaji au kuchukua hatua dhidi ya mtumiaji.
Tafadhali kagua "Matumizi Inayokubalika ya Huduma Yetu" kwenye Masharti ya Huduma kwa uangalifu ili ujifunze zaidi kuhusu matumizi sahihi ya WhatsApp na shughuli zinazokiuka Masharti ya Huduma yetu.
Tunafanya kazi kwa bidii kupunguza jumbe zozote za barua taka ambazo hupitia kwenye mfumo wetu. Kujenga nafasi salama kwa watumiaji kuwasiliana na wengine ni kipaumbele kingine. Hata hivyo, kama SMS au simu za kawaida, inawezekana kwa watumiaji wengine wa WhatsApp ambao wana namba yako ya simu kuwasiliana nawe. Kwa hivyo, tungependa kukusaidia kutambua na kushughulikia jumbe za barua taka na utapeli.
Jumbe za barua taka na utapeli zinaweza au kutoweza kutoka kwa waasiliani wako. Aina hizi za jumbe zinaeneza habari za uongo na zimeundwa kukudanganya na kukushawishi kutenda kwa namna fulani. Ikiwa ujumbe unaonekana kama tuhuma au unaonekana kuwa mzuri sana kuwa wa kweli, usiguse, usishirikishe au usiusambaze.
Tahadhari jumbe zinazo:
Ikiwa unapokea ujumbe kutoka kwa namba isiyojulikana, utapewa fursa ya kuripoti namba kwa WhatsApp moja kwa moja kutoka kwenye programu.
Kama umepata barua taka kutoka kwa mwasiliani, futa ujumbe na usibofye viungo vyovyote au kutoa taarifa za kibinafsi. Mwambie mwasiliani kuwa ujumbe aliotuma una barua taka na kumuelekeza kwenye ukurasa huu wa usalama wa WhatsApp.
Unaweza pia kutuma ripoti kwa WhatsApp kwa kuwasiliana na sisi kutoka ndani ya programu.
Ikiwa unasikia wewe au mtu mwingine yeyote yuko hatarini, tafadhali wasiliana na huduma za dharura za eneo lako.
Ikiwa unapokea maudhui kutoka kwa mtu ambaye anataka kujidhuru mwenyewe, na unajali kuhusu usalama wao, tafadhali wasiliana na huduma za dharura za eneo lako au simu ya kuzuia kujiua.
Ukipokea au ukikutana na maudhui yaliyoonyesha unyanyasaji au unyonyaji wa mtoto, tafadhali wasiliana na Kituo cha Kitaifa cha Watoto Waliopotea na Wanaonyanyaswa (NCMEC).