Usishirikishe msimbo wako wa uhakiki kwa SMS ya WhatsApp na wengine, hata kama ni marafiki au familia. Ikiwa umeshawishiwa kushirikisha msimbo wako na kupoteza upatikanaji wa akaunti yako ya WhatsApp, soma maagizo hapa chini ili urejeshe akaunti yako.
Ikiwa unamshutumu mtu mwingine anatumia akaunti yako ya WhatsApp, unapaswa kuwajulisha familia na marafiki kama mtu huyu anaweza kukuiga katika soga na vikundi. Tafadhali kumbuka, WhatsApp imefumbwa mwisho-kwa-mwisho na jumbe zimehifadhiwa kwenye kifaa chako, kwa hivyo mtu ambaye anatumia akaunti yako kwenye kifaa kingine hawezi kusoma mazungumzo ya zamani.
Ingia WhatsApp na namba yako ya simu na thibitisha kwa kuingiza msimbo wa tarakimu-6 unayopokea kupitia SMS. Jifunze zaidi kuhusu kuthibitisha namba yako ya simu kwenye Kituo chetu cha Msaada: Android | iPhone | Windows Phone.
Mara tu unaingiza msimbo wa tarakimu-6 ya SMS, mtu anayetumia akaunti yako atatolewa kiotomatiki.
Unaweza kuulizwa kutoa msimbo wa uhakiki wa hatua-mbili. Kama hujui msimbo huu, mtu anayetumia akaunti yako labda amewezesha msimbo wa uhakiki wa hatua-mbili. Ni lazima ungoje siku 7 kabla ya kuingia bila msimbo wa uhakiki wa hatua-mbili. Bila kujali kama unajua msimbo huu wa kuthibitisha, yule mtu mwingine ametolewa kwenye akaunti mara tu ulipoingiza msimbo wa tarakimu-6 ya SMS. Jifunze zaidi kuhusu uhakiki wa hatua-mbili kwenye makala hii.