Jinsi ya kubadilisha mipangilio yako ya faragha

Kimsingi, WhatsApp huweka mipangilio yako ya faragha kurusuhu:
  • Mtumiaji yeyote kuona picha ya jalada lako, maelezo kuhusu na taarifa za kusomwa
  • Unaowasiliana nao kuona masasisho yako ya hali
  • Mtumiaji yeyote kukuongeza kwenye vikundi
Kumbuka: Watumiaji uliowahifadhi kama anwani au ambao uliwatumia ujumbe hapo kabla wanaweza kuona mara yako ya mwisho kuona au kuwa mtandaoni.
Kubadilisha mipangilio ya faragha
  1. Kwenye:
    • Android: Gusa Chaguo zaidi
      > Mipangilio > Faragha.
    • iPhone: Gusa Mipangilio > Faragha.
    • KaiOS: Bonyeza Chaguo > Mipangilio > Akaunti > Faragha.
    • Desktop: Bofya Menyu
      > Mipangilio > Faragha.
  2. Unaweza kubadilisha anayeweza:
    • Kuona Mara yako ya Mwisho Kuonwa au Kuwa Mtandaoni
    • Kuona Picha ya Jalada lako
    • Kuona maelezo yako ya Kuhusu
    • Kuona masasisho yako ya Hali
    • Kuona Taarifa za kusomwa
    • Kukuongeza kwenye Vikundi
Kumbuka:
  • Usiposhiriki maelezo ya mara yako ya mwisho kuonwa au kuwa mtandaoni, hutaweza kuona maelezo ya mara ya mwisho watumiaji wengine walipoonwa au kuwa mtandaoni.
  • Ukizima taarifa za kusomwa, hutaweza kuona taarifa za kusomwa kutoka kwa watumiaji wengine. Taarifa za kusomwa hutumwa kwa soga za vikundi kila mara.
  • Ikiwa unayewasiliana naye amezima taarifa za kusomwa, hutaweza kuona ikiwa ameona sasisho lako la hali.
  • Watu waliopo mtandaoni kwenye mazungumzo ya soga nawe wanaweza kuona unapoandika.
Je, hili linajibu swali lako?
Ndiyo
La